KUWA KIOO KWA MKEO..!
Mwl Ntogwisangu JC. Watsap (0712463344)
▫Leo tunaendelea na sehemu ya PILI ya somo letu la namna ya kujiandaa kuwa mume na baba bora wa familia.
🔹Mwanamke asili yake ni kujiremba na kutaka kuonekana mzuri na mwenye mvuto Katika jamii na hasa mbele ya mwanaume.
🔹Hutumia
muda mwingi sana kujiremba na kukaa kwenye Kioo. Hubadilisha mitindo ya
nywele karibu kila wiki, mara Leo kaweka wigi kesho kasuka yeboyebo
sijui zile za mmasai ili mradi tu aonekane kapendeza na mwenye mvuto
machon pa watu.
🔹Wakati
mwingine atanyoa nyusi na kujichora na penseli yaani Mwili unakuwa kama
daftari, wenyewe huwa wanaita wanja, atapaka marangi mdomoni, kwenye
kucha, kope bila kusahau ule unga mweupe wanaopaka usoni unajulikana pia
kwa jina la poda.
🔹Yote
haya ni ili tu ajisikie kuwa ni wa thamani machoni pa watu. Ndio maana
wengine humuita mwanamke ni pambo, unajiuliza pambo la nini? Ni pambo la
Mwanaume.
🔹Sasa
hapa ndipo nataka wanaume waelewe kitu, vurugu zoote hizo za kujikwatua
anazofanya ni kwa ajili yako, ndio ni kwa ajili yako na si mtu
mwingine.
🔹Ndio
maana wanawake wengi Baada ya kuolewa zile mbwembwe za kujikwatua huwa
zinapungua kama sio kuisha na wanabaki wa kawaida, sasa kama
ulidanganywa na poda hapo Kazi unayo.
🔹Na
huwa najiuliza kama wanawake wangekuwa peke yako, hivi hizi vurugu za
kushindana mitindo hivi zingekuwepo kweli? Sijui, lakin sidhani kama
zingekuwepo. Na hata kama zingekuwepo isingekuwa kwa kiasi hiki.
🔹Sasa
kama mwanaume ni vizuri ufahamu hili, unapoona anatumia pesa nyingi
kujiremba na kununua vitu visivyo na ulazima sana, usiwe na hasira
ukaanza kumfokea na kumwona hafai. La hasha..! Hiyo ndio asili yake.
🔹Unachotakiwa
kufanya ni kufahamu psychology yao na kuenda naye polepole, Biblia
inasema tukae nao kwa akili (1 Petro 3 :7). Sasa naomba nikupe kidogo
hiyo akili ya kuchukuliana nao.
🔹Hapa
unatakiwa kucheza na AKILI yake na kuanza kumsifia kila anapotaka
kutoka au anapobadili mtindo mpya wa nywele, we mwambie "waaoh,
umependeza sana mke wangu", "you look so beautiful my dear "na maneno
mazuri kama haya.
🔹Na
kama siku amesuka nywele zile za kawaida au amevaa simple sana, hapo
sasa ndio unakoleza sifa mpaka basi," yaaan mke wangu aisee
ulivyopendeza Leo sijawahi ona yaaan acha tu" anaweza asikuamini akaona
kama unamtania lakini wewe koleza zaidi sifa na kuonesha msisitizo siku
hiyo mtoe 'OUT' mkanywe hata Soda.
🔹Unaweza
usielewe kwanin nakuambia ufanye hivi. Subir nikuambie psychology
nyingine ya mwanamke ni kupenda sana KUSIFIWA yaani hata kama hajala
kitu anaweza kujiona ameshiba.
🔹Unapomsifia
unajenga hali ya KUJIAMINI ndani yake na kujiona kuwa ni mzuri, pale
anapohisi ajapendeza muambie umependeza sana, hii itamfanya aanze
kujikubali, kujipenda na kujiona wa thamani.
🔹Wanawake
ambao wanajiremba kupita kiasi wengi wao husumbuliwa na kuwa na 'Low
self esteem' nikimaanisha hali ya kutokujikubali na kujiamini. Na dawa
ya ugonjwa huu ni KUMSIFIA TU wala hahitaji Panadol wala kukemea Pepo.
🔹Nimekuibia
Siri hii, ebu itumie na uone mabadiliko. Anza kumsifia kila siku
anapotaka kutoka, anapobadili mitindo yake ya nywele au Nguo, akiwa
anajiangalia kwenye Kioo basi kaa mbele yake msaidie kumtengeneza vizuri
na mwambie 'Nakupenda sana mke wangu mzuri', 'umependeza sana' ,
'Nashukuru Mungu kunipatia mrembo kama wewe' .
🔹Hivi
ndivyo Mwanaume anapaswa kumfanyia mke wake, na si kumkaripia na
kumtolea maneno mabaya, eti kisa anatumia pesa nyingi kujiremba,au kwa
sababu anakuchelewesha kila mnapotaka kutoka.
🔹Jenga
utamaduni wa kumsifia, amfanye ajiamini na ajione ni wa thamani,
Usiruhusu aanglie Kioo anapojiandaa, ebu fanya wewe ndio Kioo chake kwa
kumuandaa kisha mwambie kuwa Umependeza.
🔹Yale
Masaa ya kukaa kwenye Kioo yatapungua na hali ya kujiremba kama kinyago
pia ITAKOMA.. Hii ndiyo TIBA YA ASILI isiyohitaji mzizi wowote zaidi ya
nyama ya ulimi (maneno matamu).
🔹Imeandikwa.... "ENYI WAUME WAPENDENI WAKE ZENU, KAMA KRISTO ALIVYOLIPENDA KANISA AKAJITOA KWA AJILI YAKE"
"VIVYO HIVYO IMEWAPASA WAUME NAO KUWAPENDA WAKE ZAO KAMA MIILI YAO WENYEWE "
WAEFESO 5 :25, 28
🔹Naomba niishie hapa kwa Leo, tutaendelea wakati mwingine.. 👋👋
♥ BE GENTLY TO YOUR WIFE & TREAT HER PATIENTLY, SINCE SHE IS YOUR BODY AND SOUL.
MWL JOHN CHARLES NTOGWISANGU
👉KUJIUNGA NA MAGROUP YA WATSAP 0625063205, 071300654
- Blogger Comment
- Facebook Comment
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
Powered by Blogger.





0 comments:
Post a Comment